Mtandao wa Twitter unafanyia marekebisho sheria zake ili kuwarahasishia
kazi watumiaji wake na kuufanya uwe wa kuvutia kwa wale wanaojiunga nao
kwa mara ya kwanza.
Wanachama wa mtandao hao sasa wataweza kuongeza kile wanachochapisha
kwenye mtandao huo, zikiwemo picha na video bila ya kuathiri kiwango cha
sasa cha maneno 140 ambayo mtu anastahili kuandika.
Twitter pia itafanya marekebisho kuhusu jinsi watu wanaweza kuwasiliana katika mtandao.
|
Twitter imekuwa na wakati mgumu kuwavutia watumiaji wapya suala ambalo linatajwa kuchangiwa na ugumu ulio katika kuutumia. |
Mwanzilishi mwenza wa Twitter na mkurugenzi mkuu Jack Dorsey, aliiambia
BBC kuwa lengo lao ni kuhakikisha kuwa wakati watu wanapoutumia
unaonekana kuwa ulio na maana.
Mdadisi mmoja anasema kuwa hatua hizo zinaashiria mwelekeo mwema, lakini
akaongeza kuwa wameangazia suala moja tu ambalo ni kuongeza watumiaji
wake.
Licha ya mtandao huo kutumiwa sana katika masuala yanayohusu habari
mwaka uliopita, umekuwa na wakati mgumu kuwavutia watumiaji wapya suala
ambalo linatajwa kuchangiwa na ugumu ulio katika kuutumia.
|
Twitter pia itafanya marekebisho kuhusu jinsi watu wanaweza kuwasiliana katika mtandao.
|
Brian Blau, ambaye ni mchambuzi kutoka shirika la Gartner, anasema
matatizo yanaoikumba Twitter kuwapata watumiaji wapya hayawezi
kutatuliwa na mabadiliko hayo.
Anasema kuwa tatizo kuu ni kuwavutia watumiaji wapya na kuwafanya wawe
wazalendo kwa mtandao. Anaendelea kusema kuwa bado Twitter
haijalishughulikia hilo.
Source: BBC